Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa hafla ya uzinduzi wa meli ya kwanza ya Uvuvi wa bahari kuu ambayo itaiwezesha nchi kuvua samaki waliopo kwenye ukanda wa maalum wa uchumi wa bahari (EEZ) ambao awali haukuweza kufikiwa kutokana na kukosekana kwa meli ya aina hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua meli ya kwanza ya Uvuvi wa bahari kuu ambayo itaiwezesha nchi kuvua samaki waliopo kwenye ukanda wa maalum wa uchumi wa bahari (EEZ) ambao awali haukuweza kufikiwa kutokana na kukosekana kwa meli ya aina hiyo.
Ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo katika Makao Makuu ya TAFICO Ras Mkwavi, Kigamboni Dar es Salaam iliyofanyika 13 Machi 2026
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena (katikati) akitoa maelekezo wakati akipokea mradi wa ukarabati wa gati la kuegeshea meli (floating jetty) wa TAFICO, uliopo Makao Makuu ya Shirika Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam Februari 15, 2026. Kushoto kwake waliopo mstari wa mbele ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh, na kulia kwake waliopo mstari wa mbele ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TAFICO CPA Shaibu Matessa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh (wa tatu kulia) akiwa na Menejimenti ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), alipotembelea Makao Makuu ya Shirika hilo yaliyopo Ras Mkwavi–Kigamboni, jijini Dar es Salaam kukagua utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa gati la kuegeshea meli (floating jetty) na maandalizi ya ujio wa meli ya uvuvi ya Shirika kwenye ziara aliyoifanya Februari 10,2026. Kulia kwake ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu TAFICO Bi. Perpetua Massaga.
TAFICO FV. 01, meli mpya ya uvuvi ya TAFICO
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (katikati) kwenye picha ya pamoja na viongozi na watendaji wa wizara, menejimenti na watumishi wa TAFICO, alipotembelea Makao Makuu ya TAFICO Disemba 05, 2025
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (katikati) kwenye picha ya pamoja na viongozi na watendaji wa wizara, menejimenti na watumishi wa TAFICO, alipotembelea Makao Makuu ya TAFICO Disemba 05, 2025
Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi TAFICO 08 Aprili 2025
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akizindua mtambo wa kuzalisha barafu za tofali (block ice) wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), tarehe 07 Machi 2025, Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni Dar es Salaam.