MIRADI
MIRADI
Katika kuvutia uwekezaji wa serikali na sekta binafsi Mpango wa Biashara (Business Plan) wa Miaka 10 umeandalia,mpango huu umeainisha miradi ya kimkakati kwa ajili ya kuongeza tija katika uvuvi wa Bahari kuu na mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi . Miradi hii itekelezwa kwa kushirikiana na sekta binafsi kwa utaratibu wa Ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (Public -Private Partnership- PPP). Miradi hii itaiwezesha TAFICO kurejea katika shughuli za uzalishaji na kuimarisha sekta ya uvuvi nchini.
- Uvuvi wa Bahari Kuu kwa kutumia meli vya mishipi (Long Liner)
- Uvuvi wa Bahari Kuu kwa kutumia meli ya wavu wa kuzungusha (Purse Seine)
- Mradi wa uchakataji wa Mazao ya Uvuvi.
- Mradi wa uzalishaji barafu.
- Mradi wa ghala la ubaridi la kuhifadhia mazao ya uvuvi.
- Mradi wa utotoleshaji vifanga vya Samaki.
- Mradi wa uzalishaji wa chakula cha Samaki waafugwao.
- Mradi wa ufugaji wa Samaki kwenye vizimba. na
- Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwenye mabwawa