Bw. Ramadhan M. Seleman
Bw. Ramadhan M. Seleman
Kaimu Meneja wa Kitengo cha Operesheni za Uvuvi
Barua pepe: ramadhani.selemani@tafico.co.tz
Wasifu
Bw. Ramadhan Seleman Mtabika ambaye kwa sasa ni Kaimu Meneja wa Operesheni za Uvuvi wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), ni mtaalamu wa masuala ya uvuvi na ukuzaji wa viumbe maji. Uzoefu wake unatumika katika kupanga, kusimamia na kutekeleza ratiba na aina mbalimbali za shughuli za uvuvi, kuweka kumbukumbu za mara kwa mara za zana za uvuvi, vyombo vya uvuvi na wafanyakazi; kuandaa ratiba za matengenezo na usafi wa zana za uvuvi; pamoja na kupata vibali vinavyohitajika ili kutekeleza shughuli za uvuvi.
Bw. Mtabika hapo awali alifanya kazi kama Meneja wa Udhibiti wa Ubora katika Kampuni ya DONAR LTD, Mkuu wa Udhibiti wa Ubora katika kampuni ya Alpha Groups (TANPESCA LTD), Mshauri wa Kiufundi wa Wilaya katika Mradi wa Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Pwani (MACEMP) uliokuwa ukifadhiliwa na wafadhili katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa. Pia amefanya kazi kama mshauri katika kutoa mafunzo na ushauri kwa vikundi vya COCOBA, ikiwa ni pamoja na mafunzo ya wakufunzi (TOTs) na watendaji wa BMU COCOBA, pamoja na majukumu mengine ya kitaalam katika tasnia ya uvuvi.
Bw. Mtabika ana Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Afya ya Rasilimali za Viumbe Maji na Shahada ya Kwanza ya Sayansi ya ukuzaji viumbe maji. Amefunza zaidi ya wavuvi 500 kuhusu mbinu za uvunaji wa rasilimali za baharini zinazohamasisha matumizi endelevu ya rasilimali hizo, na amefanya tafiti kuhusu maambukizi ya fangasi yanayoathiri samaki jamii ya tilapia katika kituo cha utafiti cha Taasisi ya Sayansi ya Bahari (Institute of Marine Science) kilichopo Pangani, Tanzania.